Friday, September 25, 2009

JINSI YA KUTOA MIMBA KWA KUTUMIA VIDONGE VYA MISOPROSTOL





Yafuatayo ni maelekezo kuhusu matumizi ya vidonge vya Misoprostol (vidonge hivi hupatikana kwa majina ya Misotac, Citotec au Kontrac):

* Tahadhari za kuchukua
* Jinsi gani vidonge hivi vinatumika
* Vipimo bora vya dawa na matumizi yake
* Matokeo gani wanawake watarajie
* Madhara/matatizo yanayoweza kujitokeza


Kutumia vidonge vya Misoprostol (Misotec, Cytotec au Kontrac) peke yake hufanikiwa kutoa mimba kwa asilimia 80 hadi 90. Taarifa hii inatokana na utafiti uliofanywa na Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO).


Baadhi ya wanawake hujaribu kutoa mimba kwa kuingiza vifaa vyenye ncha kali au vitu vichafu tumboni au kwa kujipiga makonde tumboni. Vitendo hivi ni hatarishi na kamwe mwanamke yeyote asifanye hivyo, kwa kuwa vinaweza kusababisha majeraha yenye athari kubwa tumboni, ikiwa pamoja na kuvuja damu nyingi na hivyo kuleta kifo.

Maamuzi ya kutoa mimba ni jambo gumu sana kwa wanawake walio wengi. Iwapo huwezi kumweleza muhudumu wako wa afya kuhusu kutoa mimba au njia nyinginezo, tunashauri ujadili suala hilo na rafiki unayemwamini au ndugu wa karibu. Haswa tunashauri binti au wasichana kuongea na wazazi /mzazi wao/wake au mtu mzima anayemwamini kuhusu hali yake, uamuzi alionao na jinsi ya kutekeleza utoaji mimba.

Iwapo mwanamke yeyote anadhamira ya dhati ya kukatiza mimba yake na hana njia nyingine ya kumwezesha kufanya hivyo, ni vyema asome kwanza maelekezo haya kwa makini.

Ni vyema pia iwapo atayajadili na mmoja kati ya marafiki zake. Wala usijaribu kutekeleza jambo hili peke yako.
gonga hii link a kuendelea...JINSI YA KUTOA MIMBA KWA KUTUMIA MISOPROSTOL na TAADHARI ZA KUCHUA

0 comments: