Wednesday, February 3, 2010

Vidonge vya kuzuia mimba baada ya siku 5 vyaingia madukani


Vidonge vya kuzuia mimba kwa dharura (the morning after pills) zimeingia madukani, ambapo inaaminiwa dawa hizo zina uwezo wa kumzuia mwanamke asipate mimba hata baada ya kuzitumiwa ikiwa siku 5 tayari zimepita baada ya kujamiina. Uchunguzi uliofanywa na wataalamu wa Uingereza umegundua kuwa, daw ahizo mpya zina uwezo zaidi wa kuzuia mimba kuliko zile za zamani ambazo zilikuwa zikizuia mimba hadi baada ya siku tatu tu toka wakati wa kufanya mapenzi. Kwa kawaida dawa za kuzuia mimba kwa dharura au emergency contraception zinatumia homoni ambazo aidha huzuua yai lizitoke katika ovari masaa kadhaa baada ya kujamiiana, au kuzuia yai lisijikite katika mfuko wa uzazi. 

Si vibaya hapa nielezee vidonge vya kuzuia mimba kwa dharura ni dawa za aina gani?

The Morning after pills ni vidonge ambavyo huzuia mtu asipate mimba iwapo hakutumia njia yoyote ya kuzuia mimba kabla au wakati wa kufanya tendo la ndoa. Ingawa dawa hizo zinajulikana kwa vidonge vinazotumiwa asubuhi kama lilivyo jina lake lakini kihakika dawa hizo huwa na uwezo wa kumzuia mtu asipate ujauzito kwa muda wa masaa 72 au siku 3 kwa kawaida (Huku zile mpya nilizoungumzi hapo juu zikiweza na uwezo wa kuzuia mimba hadi siku 5). Lakini dawa hizo kila zinapotumiwa mapema zaidi baada ya tendo la ndoa, matokeo yake huwa bora zaidi. Vidonge hivyo hufanya kazi vizuri zaidi vinapotumiwa katika masaa 12 baada ya kufanya mapenzi bila kujikinga. Dawa hizo huwa zina homoni inayoitwa Lovenorgestrel ambayo ni moja ya vitu vilivyoko katika vidonge vya kawaida vya kuzuia mimba (contraceptive pills). Unaweza kuapata vidonge hivyo katika vituo vya afya au mahospitalini. 
Uingereza na katika nchi nyingi za Ulaya vidonge hivyo huitwa 'emergency contraceptive pill' wakati Wamarekani na nchi nyinginezo huviita 'The Morning After Pill'.

Viodnge vya kuzuia mimba baada ya kujamiina kwa kawaida husaidia kwa asilimia 100 kutopata mimba, na kushindwa kwake ni kwa asilimia chache. 

Vidonge hivyo vinatumika katika masuala mbalimbali kama vile:

1. Kuwazuia kupata mimba wanawake waliofanya mapenzi bila kujikinga kabla au bila kutumia kizuizi chochote wakati wa tendo la ndoa.
2. Kwa wale waliobakwa, na kuna hatari kwamba wanaweza wakapata mimba.
3. Kwa mke na mume au wale wapenzi ambao wakati wa kujamiiana condom ilipasuka. 
4. Kwa wale waliofanya ngono zembe kwa kushawishiwa, wakiwa wamelewa au kutumia madawa ili kuwazuia wasibebe mimba. 

Kumbuka kuwa, hakuna hatari yoyote kutumia dawa hizo. Lakini ni bora upate ushauri wa mtaalamu kabla ya kutumia. Ni asilimia chache sana ya wanawake ambao hupata matatizo madogo madogo baada ya kutumia dawa hizo kama yale wanayoyapata wakati wa kutumia vidonge vya kuzuia mimba vya kawaida. Matatizo hayo ni kama vile.
Maumivu ya kichwa kidogo.
Tumbo kuuma kidogo
Maziwa kuuma kidogo.
Kuona matone ya damu kidogo.
Kujisikia kizunguzingu kidogo.
Ni muhimu pia kujua kuwa, kuna wanawake ambao hawaruhusiwi kabisa kutumia dawa hizo na hao ni wale ambao wana matatizo ya figo au wale wenye matatizo yanayoitwa porphyria.
KUMBUKA KUWA KUZUIA MIMBA NI BORA KULIKO KUTOA!
Na daima tunza Afya yako!

0 comments: