Friday, July 31, 2009

Mimba uilee wewe, mtoto umbwagie mama yako! INAHUSUUU?


Wahenga walisema, kulea mimba si kazi bali kazi ni kulea mtoto. Ni dhahiri kabla ya kuutoa msemo huo walizingatia mambo kadha wa kadha yanayoizunguka jamii nzima kulingana na hali halisi ya maisha ya binadamu na jinsi anavyotakiwa kuwajibika mbele ya familia yake husika.

Ingawaje msemo huo ulilenga zaidi katika malezi ya mtoto, lakini haina maana kwamba wahenga hawakutambua kuwa kabla ya mtoto kuzaliwa ni lazima malezi ya mimba yawepo, na vile vile kuwa kulea mimba ni kazi nzito pia, ni dhahiri hilo linaeleweka na halina mjadala.

Kwa kupitia msemo huu, wahenga walikusudia zaidi kuwaasa baadhi ya wanawake ambao mara baada ya kujifungua watoto wao salama salimini, basi habari ya matunzo na malezi kwa watoto wao hugeuka kuwa ni kitendawili kisichoteguliwa. Hawa ni wale wazazi ambao bado wanapenda kujichanganya na mambo ya kujirusha zaidi kana kwamba bado ni wasichana wadogo wasio na majukumu mazito ya kifamilia.

Kwa ujumla kwa wanafamilia wanaojali na kuthamini nini maana ya mtoto ndani ya familia yao, punde mtoto anapozaliwa, huwa ni kama nuru ya upendo na faraja kubwa ndani ya familia yao.

Kinachoshangaza hapa ni pale unapojaribu kuangalia suala hili kwa kulinganisha pande mbili tofauti, wakati upande mmoja utawaona wanafamilia wanashangilia na kumshukuru Mungu siku mtoto anapozaliwa, upande wa pili utawaona baadhi ya akinadada wakitafuta jinsi ya kuwatupa watoto wao punde wanapojifungua!

Hapa kwa kweli nashindwa kupata ulinganifu wa mawazo, hasa wa hawa akinadada, kwa kifupi binafsi inaniuma sana pale ninaposikia mtoto katupwa ama chooni au jalalani wakati familia nyingine zikikesha kusali na kumuomba Mwenyezi Mungu awajalie wapate mtoto bila mafanikio.

Tukiachana na watu wa aina hii, hoja yangu kubwa ya leo ni kuwazungumzia akinadada au akinamama ambao kwa namna moja au nyingine inaonekana kama vile kwao kulea mamba na kuzaa si tabu hata kidogo, lakini linapokuja suala la malezi, hapo ndipo inapokuwa ni mgogoro mtupu, kwa kuwa miezi michache baada ya kujifungua watoto wao salama salimini, hujifungasha na kuhamishia makazi kwa wazazi wao na baadaye huwatelekeza watoto wao huko huko kwa bibi zao na wao kuanza kukata mitaa tena mijini wakijiandaa kufyatua watoto wengine!

Nasema kufyatua watoto wengine kwa sababu suala la matumizi na malezi kwa watoto wao kwao linakuwa kama vile halipo kabisa, ila wanachokijua wao ni kubeba mimba na kuzaa tu, kazi ya kulea inakuwa ni juu ya wazazi wao.

Inashangaza sana kuona kuwa, kuna watu ambao wakishajifungua tu kila kitu huwa ni juu ya wazazi wao, yaani bibi na babu wa mtoto kana kwamba wao (akinadada) kazi yao ni kubeba mimba na kuzaa tu, suala la malezi si jukumu lao!

Na kibaya zaidi, wengi kati ya akinadada wa aina hii utawakuta wana watoto zaidi ya mmoja na kila mmoja wao ana baba yake tofauti, yaani suala la kujali na kuzingatia nyota ya kijani kwao halipo kabisa!

Hivi hao wazazi wenu ambao waliwazaa nyinyi na kuwalea kwa miaka kibao huko nyuma mnataka waendelee kulea hadi lini? Ni dhahiri enzi hizi kwao si za kulea tena, huu ni wakati wao wa kupumzika na kulelewa na watoto wao, yaani nyinyi mnaowabebesha wazazi wenu mizigo yenu ndiyo mnaotakiwa kuwahudumia wao si wao wawalelee watoto wenu.

Haipendezi hata siku moja, kujirusha ujirushe wewe, mimba ubebe wewe, kuzaa uzae wewe, vipi kazi ya kulea mtoto wako umbwagie mama yako mzazi?

Acheni hizo, mnapobeba mimba mnatakiwa mjue pia kuwa kuna kazi ya kulea mtoto mbele yenu, si kufyatua tu na kuwabwagia wazazi wenu kazi ya kulea.

Yes, you can wear a bikini!


Pregnancy is the perfect time to wear a bikini! It's the one time you can wear a bikini and not worry about sucking in your stomach!

Prego Swimwear makes supportive but sexy maternity bikinis. Belabumum bikinis are Brazilian styled and come in great prints. Maternal America makes a super cute boy bottom maternity bikini. Not quite ready for the bikini...try a maternity tankini instead. Just get out, have some fun and show off that beautiful belly!

Mazoezi magumu kwa shosti mwenye mimba changa ni hatariii


Watafiti nchini Denmark wamesema mazoezi magumu kwa mwanamke mwenye mimba changa yanaweza yakamsababishia mjamzito athari ya mimba kuharibika mara dufu.

Pia watafiti hao wamegundua kwamba kukimbia kwa taratibu yaani jogging, michezo wa mpira na michezo ya kutumia racket yote inachangia hatari ya kuharibika kwa mimba sawa na kufanya mazoezi ya masaa saba kwa wiki.

Hata hivyo serikali ya Denmark inashauri mjamzito kufanya mazoezi kama kanauni ya lazima wakati wote wa kipindi cha ujauzito.

Wajawazito acheni FEGI, SIO ISHU!


Sigara na uvutaji wake huwathiri watumiaji wake popote walipo.
Mjamzito pamoja na kujidhuru yeye mwenyewe, humdhuru pia mtoto aliye tumboni.

Wajawazito walio wavutaji huweza kuzaa mtoto mwenye uzito wa chini "kabichi" au"njiti', mtoto pia anaweza kupata matatizo ya mapafu "pneumonia" na kudhoofu afya kwa ujumla.

Vile vile hata kama mjamzito havuti sigara, wana familia wengine wanaweza kumdhuru iwapo watakuwa wanavuta.

Wanawake na watoto wengi hudhururiwa na moshi wa sigara ndani ya majumba yao.

Hasa pale baba anapomaliza nusu paketi akiwa ndani ya nyumba yao! Kina baba msiyachafue mazingira ya nyumbani iwapo hamuwezi kabisa kuacha uvutaji.

Pombe ni sumu ya viungo vinavyokuwa. Inaponywewa na mjamzito huingia katika mishipa ya damu ya mtoto kupitia "placenta".
Pombe hudhuru viungo dhaifu vya mtoto vinavyokuwa.

Watoto wanaozaliwa na wanawake walevi huwa na tatizo la ukuaji dhaifu wa ubongo hivyo kuwafanya wasiwe na akili "nzuri".

Uzito mdogo wakati wa kuzaliwa, matatizo ya moyo,figo na macho, matatizo ya mifupa pia huweza kuwapata watoto hawa.

Hata kiasi kidogo cha pombe kinatosha kabisa kuwa na madhara kwa mtoto aliye tumboni.
Ni vizuri kuacha kabisa vinywaji hivi iwapo unampenda atakayekuwa mwanao siku zijazo.

Kwa wajawazito achana na marafiki walevi na kuwa mkali kwa mume au jamaa atakayekuletea zawadi ya pombe.
Usitembelee kabisa sehemu zinazouzwa pombe, wala usikodolee macho matangazo ya pombe.

Thursday, July 30, 2009

Mtoto ajifungua mtoto mwenzie!!!


Hii sasa ni hatari inamaana mtu na akili zako kabisa unathubutu kumfanyia unyama mtoto wa mwenzio kiasi cha kumpelekea kuzaa wakati si wake. huku tunakoelekea sasa ni hatari tupu.

Wapenzi wanavyoaweza kuathirika kwa kutoa Mimba!


Wenyewe wanafanya hivyo wakitoa sababu ya kwamba eti hawajajiandaa kuwa na mtoto kwa kipindi hicho. Swali la kujiuliza ni kwamba, kama hamjajiandaa kuwa na mtoto kwanini hamkuwa makini wakati wa kufanya lile tendo la ndoa?
Kwani kondom hazikuwepo ama mlikuwa hamjui namna ya kutumia kalenda katika kuzuia mimba? Huo ni ulimbukeni na kama itatokea hivyo itaonesha wazi hamko makini katika uhusiano wenu.

Tukiachana na hilo, ni wazi kwamba kila mtu anaifahamu raha ya kuwa na watoto katika maisha hasa kwa wale walio katika ndoa. Kila mtu anapenda kuitwa baba ama mama fulani hali inayowafanya walio wengi kufanya kila linalowezekana ili mwisho wa siku waweze kupata mtoto.

Naamini sote tu watu wazima na tunaelewa wazi kwamba mtoto hawezi kupatikana kimiujiza wala kwa maneno matupu, ni lazima tendo takatifu la ndoa lifanyike tena kikamilifu.

Wataalam wa mambo ya afya wanaeleza kwamba kuna mazingira fulani ambayo yasipokuwepo hata mfanye tendo hilo usiku na mchana ni vigumu kwa mwanamke kupata mimba. Ni vizuri basi wanandoa wakajiweka karibu na watu wa afya ili kufahamu njia sahihi za kuweza kupata mtoto na kwa wakati muafaka.

Lakini sasa, licha ya kwamba raha ya ndoa ni watoto kuna umuhimu mkubwa wa kujiwekea utaratibu mzuri wa kujipatia watoto hao. Si kwasababu raha ya ndoa ni watoto basi mzae tu bila mpango.

Kuna wanaume wengine wanahusudu sana ngono. Kila wakati wanataka kutimiziwa na wake zao na tena hawako makini katika kujizuia na mimba zisizotarajiwa. Matokeo yake ni mimba mfululizo kiasi cha kumfanya mama adhoofike kiafya na pia watoto wakikuwa wakiwa hawana afya nzuri.

Kwanini msijiwekea kiwango kwamba mngependa kuzaa watoto wangapi ambao mtamudu kuwapatia huduma za msingi kutokana na kipato chenu? Kwanini mwanaume asijadili na mwenza wake juu ya watoto wao wapishane kwa umri gani ili wawe makini hata wanapokuwa wanafanya tendo la ndoa? Hayo ni mambo ya msingi yanayoweza kuwafanya muione raha ya kuwa watoto katika maisha badala ya watoto kuwa karaha ndani ya nyumba.

Hakuna kitu ambacho kinawachukiza watu kama wanandoa kufikia hatua ya kutoa mimba eti kwasababu hawakupenda wapate mtoto kwa wakati huo. Kwanini hamkuwa makini tangu awali mpaka mfikia hatua ya kukiua kiumbe ambacho hakina hatia?

Kwa taarifa yako sasa, wengi waliokuwa na tabia ya kutoa mimba kila mara, huja kupata tabu sana katika kupata mtoto pale ambapo watamhitaji na kama watampata ni kwa shida sana.

Labda nitoe tu ushauri wa bure hasa kwa wale ambao ndio kwanza wameingia katika maisha ya ndoa kwamba pamoja na wale walio katika uhusiano, mtoto ana raha zake katika maisha ya binadamu na kama utapata leo kisha ukaitoa mimba jua kwamba unajiweka katika mazingira ya kumkosa mtoto huyo katika maisha yako yote. Upo ushahidi katika hilo.

Kwa maana hiyo wale wenye tabia ya kutoa mimba watambue kwamba kwanza wanajiweka katika hatari ya kupoteza maisha yao, pili wanaweza kutopata watoto tena pale watakapowahitaji na tatu wanapata dhambi kubwa kwa Mungu kwa kitendo hicho cha kinyama. Naamini wapenzi mmenisoma vilivyo. Tuonane tena wiki ijayo .

Kibibi Elizabeth Adeney kawa "kaBritain’s oldest mum at 66" kaziii


Kibibi imona nchini Uingereza kimejifungua mtoto akiwa na umri wa miaka 66.
Elizabeth Adeney alijifungua mtoto wa kiume kwa njia ya upasuaji.

An eight-month pregnant 66-year-old businesswoman - Elizabeth Adeney of Lidgate, Suffolk - is due to become the oldestmother in Britain! As per the Sunday Mirror, the issueless divorcee, who went to the Ukraine for IVF treatment, intends giving birth to her baby at a clinic in Cambridge. 


Currently, Britain's oldest mother is Dr Patricia Rashbrook, a psychiatristwho used a donated egg from Russia to birth to her son Jude in 2006, when she was 62 years old. 

Adeney told the Sunday Mirror: "It doesn't interest me that I'm going to be the oldest mum in the country. It's not my physical age that's important - it's how I feel inside." The Managing Director of a Mildenhall, Suffolk-based firm, - which produces plastic and textile products - Adeney still works full-time, and lives in a £400,000 home in nearby Newmarket. 

Adeney's neighbors talk of her as an ambitious businesswoman who, two decades back, had a colorful marriage to Robert Adeney, the ex-Chairman of Swaine Adeney Brigg and Sons - the London-based luxury leather and hunting goods firm, which supplied horse whips to the Royal Family. The couple separated within six months, and Robert Adeney, now 70, has probably moved to the South of France. 

About Elizabeth Adeney's pregnancy, her neighbor, Mavis Rennie, said: "I think she dearly wanted somebody of her own. I think she's almost alone in the world, apart from an aunt or niece in America. She has a very small family."

Je Dawa za minyoo zinatoa mimba??


Wapendwa,
poleni sana na kazi za ujenzi wa taifa na kujitafutia mkate wa kila siku.
Ninaishi na girl friend wangu ambaye siku ni mfanyakazi wa kampuni moja jijini.

Siku kadhaa zilizopita aliniambia kuwa amepata ujauzito na anahisi una umri wa mwezi mmoja.
binafsi nilifurahishwa sana na taarifa hizo kwani sasa ka umri kamekimbia na sina hata mtoto wa kusingiziwa. Lakini mwenzangu hakuwa anaonekana amefurahishwa na jambo hilo la ujauzito wake na akanishauri kuwa atoe, nikagoma.
leo ameamka mapema sana na ameniaga kuwa anaenda kununua dawa za minyoo zinazoitwa Zentel.
Je hizo dawa haziwezi kuharibu ujauzito ?
NA NI NINI MADHARA YA DAWA HIZO KWA MTU MWENYE UJAUZITO MCHANGA KAMA HUO ?

Lile jike dume eti lajifungua Mtoto wa Pili, MAKUBWAA


Yule mwanamke-mwanaume wa Marekani ambaye alijipatia umaarufu mkubwa mwaka jana baada ya picha yake akiwa na mimba huku akiwa na midevu kusambaa duniani amerudi tena kwenye vichwa vya habari mwaka huu baada ya kujifungua mtoto wa pili. Thomas Beatie, au maarufu kama 'Mwanaume Mjamzito' amerudi tena kwenye vichwa vya habari vya magazeti baada kujifungua kwa mara ya pili mtoto wa kiume jana asubuhi.

Picha za Thomas akiwa na madevu kibao huku akiwa na tumbo kubwa la ujauzito zilikuwa maarufu sana duniani mwaka jana kiasi cha kumfanya Thomas atajwe kama mwanaume wa kwanza kupata ujauzito.

Thomas anaishi na mkewe Nancy ambaye ndiye atakayekuwa akimnyonyesha mtoto wao mpya kama alivyofanya kwa mtoto wao wa kwanza wa kike anayeitwa Susan Juliette aliyezaliwa mwezi juni mwaka jana.

Thomas alizaliwa kama mwanamke lakini baadae alibadilisha jinsia kuwa mwanaume na kufanya upasuaji wa kuondoa matiti yake huku akitumia madawa ya homone za kiume yaliyomfanya awe na madevu kama mwanaume.

Thomas hakufanya upasuaji wa kuondoa uke wake hali ambayo ilimwezesha kupata ujauzito wa mtoto wake wa kwanza baada ya kupandikizwa mbegu za kiume.

Thomas ambaye hivi sasa ana umri wa miaka 35 alisema kuwa aliamua kuzaa mtoto baada ya mke wake Nancy mwenye umri wa miaka 45 kutokuwa na uwezo wa kushika ujauzito.

"Kuwa na mtoto hakuangalii kuwa wewe ni mwanamke au mwanamme, mimi pia ni binadamu na ninahitaji kuwa na mtoto" alisema Thomas.

Nine Months - Kimemakaa


This super cute maternity tee, worn by celebrities such as Jennifer Garner and Kate Hudson, shows off your growing bump perfectly! The 9 Months Tee by NOM not only tells the world that you’re expecting but with its flattering fit and cozy cotton fabrication, it is sure to become one of your favorite maternity tops!

Wednesday, July 29, 2009

Trend Alert - Plaids


Dress your baby bump with trendy plaid pieces this season. Celebrities such as Jennifer Aniston, Ashley Olsen, and Kate Bosworth are hitting the streets in this great trend and now you can dress your growing belly in the same fun styles! Check out our favorite plaid piece - the Madrid Top by Sunner. Paired with jeans or trousers, this plaid maternity top can take you through the rest of the summer and into the fall with style!