Tuesday, September 29, 2009

Why women ask for sex!


Men talk and think a lot about sex while women desire it more often. We explore the reasons...


'Men think, while women desire.' Gone are the days when ‘demanding sex’ was considered exclusively a man's forte. Today women demand sex greater than men. And they have no qualms about getting vocal about it. “I read these funny E-mail forwards that stress on men begging for sex and women denying it. It sounds so funny to me. It’s totally the opposite in my case. While men can have a good laugh over it believing that this notion exists, I literally have to seduce my husband to get him hooked on to the act,” quips production assistant Regina Baton. And she is not alone. Many girls/women had a similar story.


We spoke to women from different backgrounds to figure out what is making them addicted to sex.

It’s physically pleasurable
Amongst all the other reasons to remain glued to sex, this is the most prominent one. Good sex satisfies your physical urge, which is very normal for anyone to experience. Psychologist Seema Naina opines, “Sex is the most basic need of any person. And I am increasingly getting cases where women are complaining that men are unable to satisfy their physical needs.”

Creates positive feelings about oneself
Ideally, great sex means you are enjoying the sexual act and participating equally. It makes you feel good about yourself, thus adding to your self esteem. Shares housewife Neelam Nehra, “When my husband comes back from a whole day at work and we have our sack session, it increases my self esteem. The very feeling that I am able to satisfy him is a great pleasure. And since I never want to go out of shape to look unappealing to my husband (and other men), it even acts as a motivation to work out and feel desirable.” Wondering why?

"Sex has healing powers. It generates positive emotions and makes one feel more confident. When a woman sees her man passionate in the act, admiring her body and moves, it infuses a lot of good feelings within her," opines psychologist Jane Makulo.

Brings them closer to their man
Physical intimacy releases hormone Oxytocin, which is also known as the love hormone. Agrees relationship expert Vandana Mitra, “I have always maintained that couples should never take sex casually. It’s a very important ingredient for any relationship to sustain. It helps couples to nurture the relationship and strengthen the bond.” So whoever said having more sex with your partner means lesser cases of infidelity, made sense.

Content developer Dinna David, “I feel a major connect with my boyfriend after we make love. I just feel like being close to him. My faith in him and our relationship grows stronger.” Prachi’s boyfriend agrees, “When she told me about the 7 days a week sex, I initially could not stop laughing. I mean, this is not the only thing we have to do. But honestly it has got us closer. I just can’t take my eyes off her even when we are moving in a crowd.”

Negates unwanted emotions/ Stress-reliever
Sex is not just a physical sensation but it’s comforting and relaxing. Call centre executive Neetu Sharma shares her experience, “Whenever I have a bad day at work, sex really helps me unwind. It totally takes the stress out of my mind and makes me feel relaxed and rejuvenated." Psychologist Reena Kapur explains why. "Sex involves a lot of deep breathing and touching and the hormones that are released during the act calm you down."

Great form of exercise
Thirty minutes of sex burns more than 85 calories. We have read it almost everywhere that sex helps in burning calories. Confirms fitness consultant Stuti Batra, “While I do not suggest giving up work outs, doubling up the session makes you drop more weight.” While this is the most deadly mix, many girls are seriously taking to it. “It may sound a little funny, but while making love I prefer to play the dominant role. It helps me burn greater calories, leaving my guy in ecstasy,” says Khadija Hussein.

Invokes passion
“Sometimes I feel like a pervert, because I find myself always thinking about my boyfriend, and what we did the night before. It gives me a kick and makes me crave for our next sack session. He thinks I am crazy, but it really happens to me,” shares call centre executive Leila.

“It is completely normal to fantasise about sex. But I have heard it can freak a guy out- we men are still adapting to the concept of women demanding sex more than us. But we love that passion,” admits psychologist Eunice.

Friday, September 25, 2009

JINSI YA KUTOA MIMBA KWA KUTUMIA VIDONGE VYA MISOPROSTOL





Yafuatayo ni maelekezo kuhusu matumizi ya vidonge vya Misoprostol (vidonge hivi hupatikana kwa majina ya Misotac, Citotec au Kontrac):

* Tahadhari za kuchukua
* Jinsi gani vidonge hivi vinatumika
* Vipimo bora vya dawa na matumizi yake
* Matokeo gani wanawake watarajie
* Madhara/matatizo yanayoweza kujitokeza


Kutumia vidonge vya Misoprostol (Misotec, Cytotec au Kontrac) peke yake hufanikiwa kutoa mimba kwa asilimia 80 hadi 90. Taarifa hii inatokana na utafiti uliofanywa na Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO).


Baadhi ya wanawake hujaribu kutoa mimba kwa kuingiza vifaa vyenye ncha kali au vitu vichafu tumboni au kwa kujipiga makonde tumboni. Vitendo hivi ni hatarishi na kamwe mwanamke yeyote asifanye hivyo, kwa kuwa vinaweza kusababisha majeraha yenye athari kubwa tumboni, ikiwa pamoja na kuvuja damu nyingi na hivyo kuleta kifo.

Maamuzi ya kutoa mimba ni jambo gumu sana kwa wanawake walio wengi. Iwapo huwezi kumweleza muhudumu wako wa afya kuhusu kutoa mimba au njia nyinginezo, tunashauri ujadili suala hilo na rafiki unayemwamini au ndugu wa karibu. Haswa tunashauri binti au wasichana kuongea na wazazi /mzazi wao/wake au mtu mzima anayemwamini kuhusu hali yake, uamuzi alionao na jinsi ya kutekeleza utoaji mimba.

Iwapo mwanamke yeyote anadhamira ya dhati ya kukatiza mimba yake na hana njia nyingine ya kumwezesha kufanya hivyo, ni vyema asome kwanza maelekezo haya kwa makini.

Ni vyema pia iwapo atayajadili na mmoja kati ya marafiki zake. Wala usijaribu kutekeleza jambo hili peke yako.
gonga hii link a kuendelea...JINSI YA KUTOA MIMBA KWA KUTUMIA MISOPROSTOL na TAADHARI ZA KUCHUA

Friday, September 18, 2009

Ushauri wa bure kwa walioa na kuolewa!



Nianze kwa kuongea nanyi wanawake wenzangu. Kimaumbile wanaume wanapenda kuona wanasikilizwa na wake zao na hawakawii ‘kukubadilikia’ unapowakwaza. Pamoja na kwamba nanyi mna sauti ndio, lakini wanaume ni watu wa kuwasoma kwanza na kuwaendea taratibu kuliko kuwapandishia na kuonesha kushindikana nao. Kama kweli unampenda basi muoneshe unamheshimu, hapo utampata!

Wanaume hupenda wanawake wasafi, wakarimu, wacheshi na wasio na kiburi wala ‘nongwa’ zisizokuwa na maana, jitahidi katika hayo ili ukonge moyo wa mpenzi wako na kamwe hatakusaliti.

Lakini huwa nasikitishwa sana na hizi zama za usawa ambazo zinachochea migogoro mingi katika ndoa. Kwa mfano, hivi sasa mwanamke kumtii mumewe kunachukuliwa ni kama utumwa!

Nawahakikishia, kwa ninavyofahamu hisia za wanaume walio wengi, hali hii ikiendelea sidhani kama kutakuja kuwa na mapenzi imara, sana sana mapenzi yatageuka kuwa uwanja wa mapambano na ushindani siku zote.

Nawaomba wanawake, pamoja na elimu mliyonayo na visomo vya hali ya juu, jitahidini kujilazimisha kuwaheshimmu waume zenu kwani kamwe hamtapungukiwa na kitu bali mtajihakikishia mapenzi yenye utulivu na amani siku zote za maisha yenu!

Nikiwageukia wanaume, jamani akina kaka na akina baba, ninyi mnachukua nafasi ya baba yenu Adamu. Baba yetu Adamu alimpenda mke wake kwa dhati hata akashawishika kula tunda alilokatazwa ili mradi asimsononeshe mkewe.

Yawapasa mfahamu kuwa wanawake ni zawadi kwenu, pumziko na tulizo la mioyo yenu. Wanawake ndio raha yenu na amani kubwa ya maisha yenu.
Kosa kubwa mnalofanya wanaume ni kuutumia vibaya “mfumo dume” hasa katika suala nyeti kama mapenzi. Mapenzi si ubabe, mapenzi ni upole na ukarimu. Pamoja na kwamba mmebarikiwa kwa kupewa nafasi ya kuwa ‘kichwa katika nyumba’ lakini linapokuja suala la kurekebisha tofauti zinazojitokeza katika uhusiano wenu, si vyema kutumia njia za kibabe.

Niwaambie kitu, wanawake ni wa ‘hisia’ zaidi na waliobarikiwa upendo wa hali ya juu na ndio maana wakapewa dhamana ya kubeba mtoto tumboni kwa miezi tisa na pia kumnyonyesha na kumlea kwa miaka kadhaa, wewe ungeweza?

Nasema ni watu wa hisia kwa sababu, hivi uliwahi kufikiri ni kwanini wanawake huridhika sana na kujisikia poa kweli wanapopewa zawadi kama ya maua na kadi zenye ujumbe wa mapenzi ukilinganisha na wanaume? Unafikiri ni kwanini wana machozi ya haraka wanapotendwa? Au unafikiri ni kwanini wanapenda kutumiwa meseji za kimah aba ‘love message’ zaidi kuliko kupigiwa simu? Jiulize.

Mimi nawaona wanawake kama watu wa kuheshimiwa na kupendwa sana. Mkumbuke wanawake ndio mama zetu, walezi wetu na ndio nyumba zetu. Ridhika na mpenzi uliye naye, heshimu hisia zake na thamini mapenzi yake kwako na mpe ile kitu roho inapenda!

Tuesday, September 15, 2009

Chanjo mpya ya kansa ya mlango wa uzazi (Cervical Cancer) yagunduliwa



Mashosti wanasayansi hivi karibuni wametengeneza chanjo mpya ambayo inazuia virusi vinavyosababisha saratani ya mlango wa uzazi au cervical cancer.

Chanjo hiyo iliyotengenezwa na shirika la Glaxo SmithKline inaweza kuzuia aina mbalimbali za virusi kwa karibu asilimia 93, vinavyoweza kusababisha kensa ya mlango wa uzazi. Matumizi ya chanjo hiyo mpya hayana athari zozote mbaya muhimu kwa mtumiaji, isipokuwa maumivu kidogo na uvimbe sehemu inapochomwa dawa.

FDA imesema kuwa chanyo hiyo inaweza kutumiwa kwa wanawake wenye umri wa miaka 10 hadi 25.

Ugonjwa wa kansa ya mlango wa uzazi unasababishwa na virusi vya Papilomma (HPV) ambapo aina 15 za vijidudu hivyo huweza kusababisha ugonjwa huo. Kensa ya mlango wa uzazi ni kensa ya tano miongoni mwa saratani zinazosababisha vifo vya wanawake ulimwenguni, ambapo wanawake karibu 473,000 hupatwa ugonjwa huo kila mwaka.

Inasemekena kuwa karibu asilimia 85 ya vifo vya wanawake katika nchi zinazoendelea vinasababishwa na kensa ya mlango wa uzazi. Nchini Marekani pekee wanawake 11,999 hupata ugonjwa huo na serikali kutumia karibu dola bilioni 2 kwa ajili ya matibabu ya ugonjwa huo kwa mwaka.

http://www.presstv.ir/detail.aspx?id=105373§ionid=3510210

Kushare kitanda na laaziz sio kuzuri kwa afya


Wataalamu wanasema kulala kitanda kimoja na mpenzio si kuzuri kwa afya yako!

Wapenzi wanashauriwa kufikiria kulala vitanda tofauti, kwani kufanya hivyo ni vizuri kwa afya na uhusiano wao.

Mtaalamu wa masuala ya usingizi Dakta Neil Stanley amesema katika Warsha ya Sayansi ya Uingereza jinsi kulala kitanda kimoja wapenzi kunavyoweza kusababisha mapishano juu ya kukoroma na hata kugombaniana shuka usiku uliopita.

Utafiti umeonyesha kwamba, kwa wastani wapenzi wanakabiliwa kwa asilimia 50 na matatizo ya usingizi pale wanapolala kitanda kimoja.

Mtaalamu huyo ambaye analala mbali na mkewe, amesema kuwa kihistoria hatukutakiwa kulala kitanda kimoja. Ameelezea kuwa, desturi ya kisasa ya vitanda vya harusi ilianza tu wakati wa mapinduzi ya viwanda, ambapo watu walianza kuhamia kwenye miji na vitongoji vyenye misongamano ya watu na hapo ndipo walipojikuta wanakabiliwa na uhaba wa nafasi. Anaendelea kueleza kuwa, kabla ya kipindi cha Vitoria haikuwa imezoeleka kwa waliooana kulala pamoja.

Na wakati wa Urumi ya zamani, vitanda vya harusi vilikuwa ni sehemu ya kukutana kimwili lakini si kwa ajili ya kulala. Kwa hivyo Dkt Stanley amesema kuwa, watu hivi sasa wanatakiwa kufikiria kufanya hivyo.

Naye Dkt Robert Meodows ambaye ni mtaalamu wa elimu ya Sosholojia katika chuo kikuu cha Surrey anasema, watu wanafikiri wanalala vizuri zaidi wakati wakilala na wenzi wao, lakini ushahidi unaonyesha kinyume chake.

Uchunguzi uliofanywa kwa kuwashirikisha wapenzi 40 umeonyesha kuwa, wakati wenzi wakilala kitanda kimoja, na iwapo mmojawapo anahangaika hangaika wakati wa usingizi, kuna uwezekano kwa silimia 50, mwenzi wake akasumbuka kutokana na hali hiyo.

Uchunguzi huo umegundua kuwa, hata hivyo wapo wenzi wanaolala vitanda tofauti lakini wachache, huku wale walio kwenye umri wa miaka 40 au 50 kwa asilimia 8 hulala vyumba tofauti.

Monday, September 14, 2009

CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE!


Mwambie, usione haya



Zamani ilikuwa ni wanaume waliokuwa wakilalamika, kwamba wake zao hawataki kuwapa chakula cha usiku kama wanavyotaka. Lakini baadae yaani siku hizi ni zamu ya wanawake kulalamika.

Katika nyumba nyingi siku hizi hasa mijini wanawake ndio wanolalamika zaidi kukosa chakula cha usiku kama wanavyotaka kutoka kwa waume zao.

Kwa nini hali hii?

Ukweli ni kwamba maisha yamebadilika sana na kila mtu anajitahidi sana kutaka kuhahakisha kwamba anafanya kazi hadi anaishiwa nguvu kabisa, akili na mwili vinachoka. Wanaume wengi wanaolalamikiwa na wake zao kuhusu kupata uhaba wa chakula cha usiku ni wale wanaofanya kazi sana.

Ningependa kuwashauri wanaume kwamba wakati wanafanya kazi zao mchana wakumbuke kwamba kuna wake zao wapendwa ambao wanawasubiri jioni kuzungumza nao na zaidi ya hapo. Wakumbuke hawajaoa kazi bali wameoa wake.. Pamoja na kwamba ni muhimu kwao kufanya kazi, lakini wakumbuke kwamba kazi hazina mwisho.

Kuna jambo ambalo wanaume na hata wanawake hawalijui vizuri, hili ni lile linalohusu mazoezi. Mtu anapofanya mazoezi anawezesha damu kuzunguka na kufikia sehemu zote za mwili kwa kiwango kinachotakiwa. Kukaa ofisini kutwa na kurudi nyumbani na kukaa kwenye kochi na kuangalia TV siyo aina ya maisha inayoshauriwa tuishi. Mwili unapochangamka kwa damu kufika kila mahali kwa kiwango kinachotakiwa hamu ya kutoa chakula cha usiku na kukipokea huwa kubwa.

Lakini mbaya zaidi ni kwa wanawake wenyewe pia.. Kuna wanawake ambao bado wanaishi kwa miiko ya karne moja nyuma. Hawa wanangoja wanaume zao wawachokoze, wasipofanya hivyo, basi hata mwaka watakaa wakilalamika kwamba hawapati chakula cha usiku. Tukumbuke kwamba hata wanaume nao ni binadamu pia, huhitaji wakati mwingine kushtuliwa, kwani wakishtua wao tu kila siku, kuna wakati hukinai

Wednesday, September 9, 2009

Mtoto wa Mwaka Mmoja Mwenye Mimba Awashangaza Madaktari China


Madaktari wa nchini China walishangazwa kuona mtoto wa mwaka mmoja ana ujauzito.

Mtoto Kang Mengru wa nchini China alipelekwa hospitali baada ya wazazi wake kushtushwa na hali ya tumbo lake kuzidi kuwa kubwa siku hadi siku.

Baada ya mtoto huyo kufanyiwa ultrasound, madaktari waligundua kuwa mtoto huyo wa kike alikuwa amebeba kitoto kichanga kwenye tumbo lake ambacho kilikuwa kikiendelea kukua.

Madaktari wanaamini kuwa mama wa mtoto huyo alikuwa na mimba ya watoto wawili mapacha na pacha mmoja alijitokeza ndani ya tumbo la pacha mwenzake.

Hali kama hiyo ya kichanga kuzaliwa ndani ya kichanga kingine ni nadra sana kutokea na humtokea mwanamke mmoja katika wanawake 500,000.

Mtoto Kang atafanyiwa upasuaji kukiondoa kichanga hicho tumboni mwake.

Mashosti wanaogonga lager daily wako hatarini


Wanawake wanaopendelea kunywa mvinyo kila usiku wameonywa kwamba, wako katika hatari kubwa ya kukabiliwa na kensa!

Watafiti wa Kensa wa Uingereza wametangaza kwamba, kunywa gilasi moja tu ya ulevi kwa siku kunasababisha kensa 7,000 za ziada, nyingi zikiwa ni za matiti, hasa kwa wanawake wa nchi hiyo.

Hatari ya kupata ugonjwa huo inaongezeka kila unywaji unavyoongezeka, na hakuna tofauti iwapo pombe hiyo ni spirits, mvinyo au bia ya Safar Lager!. Hayo ni kwa mujibu wa watafiti hao. Takwimu zimeonyesha kuwa, kunywa pombe chupa moja kwa siku kunaongeza uwezekano wa kupata aina zote za kensa kwa asilimia 6 kwa wanawake ambao wana umri wa mpaka miaka 75.

Haya chime kina mama wanyaji, msijisahau na mjali afya zenu!
Link..
http://news.bbc.co.uk/2/hi/health/7906355.stm

Tuesday, September 8, 2009

Mazoezi ya kuondoa ndambi (Tumbo)


kiwa wewe hujawahi kuzaa nitakushauri ufanye mazoezi ya kukimbia kisha malizia na “sit-ups” mia moja kwamba hamsini asubuhi na hamsini jioni. Hakikisha unaanza mazoezi asubuhi kabla hujala kitu kinaitwa kifungua kinywa (muda mzuri kuanza ni alfajiri au asubuhi kati ya saa moja na mbili) na muda mzuri kwa mazoezi jioni ni kuanzia saa kumi, kumi namoja na saa moja kabla hujala mlo wa jioni.

Siku ya kwanza itakuwa ngumu siku ya pili mpaka wiki utapatwa na maumivu ya misuli sehemu ya tumbo, hiyo ikitokea inamaana kuwa misuli inafanya kazi na hupaswi kupumzika au kuacha

Kwa wale mama wapya; ndio umejifungua hivi karibuni ni vema ukafuata maelekezo ya Mkunga wako na watu wengine lakini kumbuka tu kuwa unakula chakula cha kukutosha wewe na sio kula kwa ajili yako na mtoto (kiasi cha maziwa kinatoka kilekile hata kama utakula mlo wa watu wanne).

Unachopaswa kuzingatia ni kula mlo kamili wenye virutubishao vyote (balance diet) kama vile wanga, mafuta, protini n.k. Pia kumbuka na kukaza tumbo lako kwa kulifunga khanga nyepesi au kitambaa chepesi ili kusaidia kurudisha tumbo lako la uzazi na kuwa kama lilivyokuwa awali kabla hujawa mjamzito.

Nashauri mazoezi haya yafanywe wiki sita au mtoto anapotoka Arobaini (kwa waislamu) baada ya kujifungua kwa njia ya kawaida na sivinginevyo, vilevile yafanywe hatua kwa hatua. Mfano leo unafanya hatua ya kwanza, kesho ya pili n.k, hivyo ni vyema kama utaandaa ratiba yako ambayo itakusaidia au kukumbusha zoezi linalofuata .

*Hatua ya kwanza ni zoezi liitwalo “maombi”na lina sehemu mbili( hukaza misuli ya tumbo na kuondoa uvimbe).

Mosi, lala chali, kunja miguu yako, hakikisha kuwa unyayo uko sambamba na sakafu. Tenganisha kidogo mapaja yako na uweke mikono yako katikati huku viganja vikiwa vimekutana, kasha nyanyua kichwa na sehemuya juu kidogo ya kifua na kurudi chini mara kumi.

Pili, ukiwa umelala hivyohivyo jitahidi kuinua kichwa hadi sehemu ya mgongo na kurudi chini mara kumi.

*Hatua ya pili nayo imegawanyika katika sehemu mbili na zoezi lenyewe linaitwa “uti” (huimarisha mgongo, hupunguza tumbo, makalio na mapaja).

Mosi, lala chali,kunja miguu yako, smbaza mikono yako huku na huko na viganja vyako vikiangalia juu.

Hakikisha miguu na magoti vimetengana kama inchi tano hivi. Vuta pumzi (usitoe) geuza kichwa chako upande wa kushoto , huku magoti, miguu na makalio vikiwa upande wa kulia. Kaa hivyo kwa dakika tatu.

Pili, Rudisha kichwa mahali kilipokuwa mwanzo na upumue, rudia tena kama awali kadri uwezavyo lakini kumbuka kubana pumzi na kutoa pumzi sehemu ya pili ya zoezi hili.

*Hatua ya tatu ni zoezi liitwalo “kunja nyonga” vilevile limegawanyika katika sehemu mbili na hukaza misuli ya tumbo na kulipunguza .

Mosi, lala chali, inua miguu juu huku mikono yako ikiwa huku na huko na viganja vikiangalia juu, kaa hivyo kwa dakika moja na kisha nenda sehemu ya pili.

Pili, Peleka miguu yako (ikwa imeinuka juu) hadi kwenye kichwa na uhakikishe kuwa makalio yako yameinuka na ukae hivyo kwa dakika mbili kisha rudisha miguu yako chini na urudie tena mara ishirini.

Sunday, September 6, 2009

KULEGEA KWA MISULI YA UKE (Vaginal prolapse)


Tatizi hili huwatokea zaidi wanawake walio kaika umri mkubwa ingawa pia linaweza kutokea katika umri mdogo.Tunapozungumzia kulegea kwa misuli ya uke hapa kuna tofauti kidogo na kutanuka kwa misuli hiyo.Tukizungumzia kulegea ina maana misuli ya ukeni inashindwa kubcana na kuachia njia.Hapa misuli inayoachia njia inapolegea hata ukichuchumaa uhisi nyama zimejaa ukeni.


Chanzo cha tatizo
Kulegea kwa misuli ya uke kutokana na matatizo mbalimbali na hasa uzazi wa karibu karibu,mama anayezaa kwa vipindi viwili vifupi vifupi kwa njia ya kawaida hupatwa na tatizo hili,kulegea kutokana na matatizo ya vichocheo (Hormones) za kike,kulegea kunaweza kusababishwa na magonjwa sugu kama kansa,TB na maambukizi ya HIV,Magonjwa ya zinaa haswa kawende pia huchangia.


Kulegea kwa misuli ya uke kutokana na matatizo mbalimbali na hasa uzazi wa karibu karibu,mama anayezaa kwa vipindi viwili vifupi vifupi kwa njia ya kawaida hupatwa na tatizo hili,kulegea kutokana na matatizo ya vichocheo (Hormones) za kike,kulegea kunaweza kusababishwa na magonjwa sugu kama kansa,TB na maambukizi ya HIV,Magonjwa ya zinaa haswa kawende pia huchangia.

Mama anayeongezwa njia, baada ya uke kutanuka pia misuli pia inalegea,ingawa uke pia unaweza kutanuka hata bila hata ya misuli kulegea.Tatizo hili la kulegea misuli pia huchangiwa na umri mkubwa kwahiyo kwa wabibi hali hii inapojitokea ni kawaida hasa kuanzia umri wa miaka 70 na kuendelea.


Dalili za tatizo
Mama mwenye tatizo hili wakati wa kujisafisha ukeni atahisi kama tundu limeziba au limejaa nyama na inabodi atumie muda kujisafisha mara kwa mara atakuwa anasumbuliwa na muasho na uchafu wa mara kwa mara wakati wa kufanya tendo la ndoa, maumivu wakati wa tendo la ndoa ambayo hutokea pale tu inapotokea michubuko na maumivu wakati wa tendo la ndoa.


Mama mwenye tatizo hili wakati wa kujisafisha ukeni atahisi kama tundu limeziba au limejaa nyama na inabodi atumie muda kujisafisha mara kwa mara atakuwa anasumbuliwa na muasho na uchafu wa mara kwa mara wakati wa kufanya tendo la ndoa, maumivu wakati wa tendo la ndoa ambayo hutokea pale tu inapotokea michubuko na maumivu wakati wa tendo la ndoa.

Tatizo ambalo huambatana na uambukizo wa muda mrefu ukeni,pamoja na mama kutojisikia wakati wa tendo la ndoa,maumivu wakati wa tendo la ndoa ambayo hutokea pale tu inapotokea michubuko,uambukizi huweza kupanda hadi kwenye mlango wa uzazi,tumbo la uzazi,mirija na vifuko vyo mayai.

Maambukizo yanapofikia huko mama huumwa na tumbo chini ya kitovu mara kwa mara,mwenendo wa siku za hedhi huvurugika kupata ujauzito.

Hali ya kulegea kwa misuli ya uke pia humuathiri hata mume kwani naye hushindwa kufurahia tendo la ndoa,kulegea na kutnuka kwa uke yote huathiri mahusiano ya kimapenzi kwani mama hafurahii na baba yake hafurahii tendo la ndoa.

Katika kutanuka kwa uke tumeona kuwa uke unatanuka zaidi ya kipenyo chake cha halali ambacho ni sentimeta nne,hivyohivyo kipenyo cha uume ni sentimeta nne.

Utawezaje kujua kama unatatizo?
Mama mwenye tatizo la kutanuka kwa uke au kulegea kwa misuli ya uke anaweza kujigundua kwa kufuatilia dalili zote.Njia nyingine pitisha vodole viwili ukeni kama vitapwaya ongeza view vitatu vikiweza kuingia vitatu au zaidi bila shida yoyote sambamba na dalili ambazo tumekwisha ziona basi ujue unatatizo hili la kulegea kwa misuli ya uke inapolegea kama tulivyoona hapo awali utahisi kitu kinajaa au kuvimba au nyama zinajitokeza ukeni unapochuchumaa.


Mama mwenye tatizo la kutanuka kwa uke au kulegea kwa misuli ya uke anaweza kujigundua kwa kufuatilia dalili zote.Njia nyingine pitisha vodole viwili ukeni kama vitapwaya ongeza view vitatu vikiweza kuingia vitatu au zaidi bila shida yoyote sambamba na dalili ambazo tumekwisha ziona basi ujue unatatizo hili la kulegea kwa misuli ya uke inapolegea kama tulivyoona hapo awali utahisi kitu kinajaa au kuvimba au nyama zinajitokeza ukeni unapochuchumaa.

Uchunguzi
Muone daktari wa magonjwa ya akina mama kwa uchunguzi na ushauri wa tiba.Vipimo mbalimbali vitafanyika kubainisha tatizo kama kipimo cha damu,vipimo vya ukeni mfano kipimo cha speculum examination,kuotesha uchafu wa ukeni,kama mama ana maumivu ya tumbo vipimo vya ultrasound pia vitafanyika,mwenendo wa mfumo homoni na historia ya tatizo kwa ujumla itafanyiwa tathimini,vilevile itasaidia kujua kama tatizo ni la kuzaliwa nalo,uzazi wa karibu karibu au ni nini.Uchunguzi huu ufanyika ili kuweza kupanga tiba ambayo huwa zaidi ya umoja ili kuweza kufanikisha.


Muone daktari wa magonjwa ya akina mama kwa uchunguzi na ushauri wa tiba.Vipimo mbalimbali vitafanyika kubainisha tatizo kama kipimo cha damu,vipimo vya ukeni mfano kipimo cha speculum examination,kuotesha uchafu wa ukeni,kama mama ana maumivu ya tumbo vipimo vya ultrasound pia vitafanyika,mwenendo wa mfumo homoni na historia ya tatizo kwa ujumla itafanyiwa tathimini,vilevile itasaidia kujua kama tatizo ni la kuzaliwa nalo,uzazi wa karibu karibu au ni nini.Uchunguzi huu ufanyika ili kuweza kupanga tiba ambayo huwa zaidi ya umoja ili kuweza kufanikisha.

Matibabu na ushauri
Tiba hutolewa katika Hospitali kubwa au katika cliniki maalum za magonjwa ya akinamama,tiba ni kurekebisha misuli hiyo kwa njia ya upasuaji mdogo na baadhi ya dawa ili kumrudisha mama katika hali ya kawaida.


Mwanamke aepuke vyanzo mbalimbali mojawapo ni uzazi wa karibu karibu hivyo afuate uzazi wa mpango uwe wa kalenda,sindano,vidole au vijiti au kitanzi.

Tiba hutolewa katika Hospitali kubwa au katika cliniki maalum za magonjwa ya akinamama,tiba ni kurekebisha misuli hiyo kwa njia ya upasuaji mdogo na baadhi ya dawa ili kumrudisha mama katika hali ya kawaida.Mwanamke aepuke vyanzo mbalimbali mojawapo ni uzazi wa karibu karibu hivyo afuate uzazi wa mpango uwe wa kalenda,sindano,vidole au vijiti au kitanzi.

Epuka kupata magonjwa au maradhi ya ukeni mara kwa mara kwa kujisafisha vizuri na unapohisi tu unatatizo ukeni haraka muone daktari anayeshugulika na magonjwa ya kinamama kwa msaada mkubwa.

Chakula bora hasa mboga za majani na matunda mara kwa mara kwa kulinda na kuimarisha mwili mojawapo ni kuweka sawa mwenendo wa mfumo wa homoni kuimarisha muonekano wa mwili na viungo vya uzazi na upevushaji wa mayai.Wahi hospitali kwa uchunguzi.

Friday, September 4, 2009

Dawa ya malaria kwa watoto yenye ladha ya Cherry


Dawa mpya ya malaria imetengenezwa na kuanza kuuzwa madukani yenye ladha ya cherry, lengo lake likiwa ni kuwafanya watoto wakubali kunywa dawa hiyo kwa urahisi. Tunajua dawa nyingi za vidonge za malaria ni chungu, suala ambalo linaleta kizuizi katika kutibiwa vizuri watoto wanaopatwa na malaria.

Watoto wengi hukataa kula dawa hizo hata baada ya kuongezwa sukari. Lakini dawa tamu inayopendwa na watoto ya malaria iitwayo Coartem inaonekana kuwa suluhisho la tatizo hilo.

Dawa hiyo huweza kuyeyuka katika maji na maziwa ya mama, lakini hunukia kama juice ya matunda ya cherry!.
Inatarajiwa kuwa dawa hiyo itaanza kutumika katika nchi za Kiafrika hivi karibuni.

Kumbuka kuwa:
Ugonjwa wa Malaria ni ugonjwa unaoua zaidi duniani, ambapo watu milioni 1 kufariki dunia kila mwaka kutokakana na ugonjwa huo. Wahanga wakubwa wa ugonjwa wa malaria ni watoto.

Tuesday, September 1, 2009

KUZUIA MIMBA KWA KUTUMIA KALENDA


Kwanza nataka niwaeleze wadau juu ya athari za vidonge vya kuzuia mimba:

Wanawake wengi hujikuta wanakumbwa na machafuko ya tumbo au kutapika wakati wa asubuhi, kuvimba matiti kama siyo kukumbwa na dalili za ujauzito mara wanapoanza kutumia vidonge kwa mara ya kwanza!Hii husababishwa na vidonge hivyo ambavyo vina hormones zile zile ambazo mwanamke huzitia kwenye damu wakati akiwa na mimba. Hata hivyo wataalam wanasema kuwa dalili hizi hufikia kikomo baada ya miezi kati ya 2 hadi 3.

Sambamba na hilo watumiaji wengine wavidonge hutokwa na damu nyingi wakati wakiwa kwenye siku zao.

Athari kubwa anayoweza kuzipata mtumiaji wa vidonge vya kuzuia mimba ni kuganda kwa damu kwenye moyo, mapafu au ubongo!

Wadau naomba muelewe kuwa kwa wanawake wengine mimba pamoja na kutumia vidonge vya kuzuia mimba vina hatari kubwa zaidi kwao. Hivyo basi wanawake hawa ni lazima watumie njia zingine za kuzuia mimba!

Baada ya kutanabaisha hayo naomba sasa nimjibu dada yangu jinsi yakutumia kalenda kujikinga na mimba!

Njia hii haina uhakika sana wa kuzuia mimba, lakini ni nzuri kwa sababu haigharimu chochote.Njia hii huwafaa zaidi wanawake amabo taratibu za siku zao za kwenda mwezini ni kawaida mara moja kila baada ya siku 28, na ili iweze kuzaa matunda, njii hii huhitaji mtumiaji awe tayari kukaa bila kukutana kimwili kwa muda wa wiki moja kila mwezi!

Kwa kawaida kuna siku 8 tu kila mwezi ambazo mwanamke anaweza kupata mimba ambapo siku hizi zipo katikati ya siku zake za kwenda mwezini, na huanza siku 10 baada ya siku ya kwanza ya kupata damu ya hedhi. Hivyo basi ikiwa mwanamke yoyote hataki kupata mimba ni lazima aache kukutana na mwanaume kwenye siku hizi 8! Naamini hili linawezekana kwani siku nyingine zilizobakia wapendanao wanaweza kujiachia kama kawaida kwani hakuna uwezekano wa mwanamke kushika mimba!

Ili kuepukana na kutatanikiwa, ni lazima mwanamke aonyeshe kwenye kalenda zile siku ambzo hatakiwi kukutana na mwanaume. Hapa inaweza kuwa ngumu kuchora kalenda ya ukutani kwa kuwa inatumiwa na wengi lakini ni rahisi kutekeleza hili kwa kutafuta pocket kalenda [kijikalenda ambacho waweza kiweka kwenye pochi yako]

Kwa mfano: Unaingia kwenye siku zako tarehe 5 Desemba, weka alama kwenye tarehe hiyo kisha hesabu siku 10 na baada ya hapo pigia msitari siku 8 zinazofuata!

Angalia mfano huu:-

Kumbuka siku hizo nane utakazozipigia msitari ni hatari kwani ukikutana na kidume tu na kushiriki ngono bila kutumia kondom utashika mimba, hivyo ni vema usikutane na mwanaume hata kidogo, yani epuka hata akikubembeleza na lugha laini kuwa nitapizia nje sweetie, sijui nini na nini kama hataki tumia kondom kataa kwani kupizia nje ni bahati nasibu hasa pale mwanamke anapoamua kumpa mwanaume maujuzi ya kabatini ambayo ni adimu, yaani mwanaume hupewa kwa sababu maalum tu hali inayomfanya apagawe kwa huba na hivyo huweza msababisha ashindwe kupiziza nje!

Nimalize kwa kusema kuwa, mwanamke anapaswa kuendelea na utaratibu huu kila mwezi lakini akumbuke kuwa, njii haina uhakika sana mbaka itumiwe sambamba na njia nyingi9ne kwama vile kondom.